SEHEMU YA NNE
KILA MTU ANA HAKI YA KUPONYWA
Ni wazi
Yesu hakufa msalabani kwaajili ya
kikundi Fulani bali kwaajili ya ulimwengu mzima kwa njia ya Imani
Kuponya ni
mapenzi ya Mungu na ndio maana moja ya jina lake Mungu ni MPONYAJI yaani Jehova
rapha
Katika
huduma nimekuja kugundua kuwa hata mpagani anaweza kupona ikiwa tu ataamini
kwamba anapona
Uponyaji
sio kwaajili ya watu waliobatizwa na kuokoka tu bali yoyote ambaye ataamini
kwamba anapona hakika anapona
Changamoto
ya mpagani ni kuwa anahitaji kuijua kweli vyema ili kulinda uponyaji maana bila
maarifa ni lazima adui atamuangamiza tena
Hosea
4:6 a “Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa’’
Ukisoma
biblia vizuri utagundua kuwa Yesu hakuwahi kubagua wa kuponya na kuacha kuponya
bali kizuizi pekee kilikuwa kutokuamini
Kwenye
injili Yesu alikutana na mwanamke ambaye ni wa mataifa au myunani(waabudu
miungu) na baada ya kuipima Imani yake akagundua wakati anafundisha alielewa na
IMANI yake ikamponya binti yake
Mathayo
15:27-28 “Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo
mezani pa bwana zao. Ndipo Yesu akajibu, akamwambia,
Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu
saa ile.’’
Huyu
Mama alikuwa wa mataifa yaani ni sawa na watu ambao hawajapokea wokovu kwasasa
au wapagani lakini tunaona Yesu anasema wazi kuwa Imani yake imemponya binti
yake
Hivyo
basi uponyaji haubagui chochote zaidi ya IMANI ya mtu
Kitu
pekee kinaweza kuzuia uponyaji ni pale ambapo mtu atapata ugonjwa kwa kujidhuru
mwenyewe kwa kutokusamehe, hapa atapaswa kusamehe ili kupokea uponyaji
Usikubali
kabisa kuona kwamba haufai kuponywa na Mungu ,hata wapagani waliponywa kwanini
wewe usiponywe
Usikubali
uongo wa shetani kwamba uponyaji ni wa dhehebu Fulani
Kuna
watu wamedanganywa kwamba ili wapone wanapaswa kubadili dhehebu ,huu ni uongo
katika uoande wa kupokea uponyaji
Dhehebu
haliwezi kuwa kizuizi cha mtu kupokea uponyaji ikiwa dhehebu hilo linamfundisha
IMANI ya kweli
Kuna
watumishi pia wanadhani kuwa dhehebu Fulani hawawezi kupona hata wakiwaombea
kitu ambacho sio kibiblia
Nilikutana
na dada mmoja ambaye wakati anaumwa lile tatizo kuna watu wa dhehebu Fulani
wakaanza kumwambia kuwa anapaswa kubatizwa tena na tena ili akiombewa apone
Huu
ni uhadaifu kibiblia
Na
kamwe hatupaswi kutumia matatizo ya watu ili kuvuta watu kwetu bali injili ya
kweli imgeuze mtu
Yesu
aliponya kila mtu aliyeamini
Lazima
tujue kuwa taifa pekee ambalo lilimuabudu Mungu wa kweli hata wakati wa Yesu
akiwa duniani ni ISRAEL na watu wa mataifa mengine walionekana wapagani
Lakini
ukisoma biblia utagundua yesu hakubagua aliwaponya hadi watu wa mataifa wale
walioamini watapona
Wafuatao
ni watu wa mataifa walioponywa katika biblia
a. Mkoma Msamaria – Luka 17:11–19
Wasamaria
walihesabiwa kama watu wa mataifa maana walikuwa matokeo ya waisrael
kuingiliana na mataifa baada ya kuvamiwa na Ashuru
wakapaza
sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!
Luka
17:14-17 “Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani.
Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika.Na mmoja wao alipoona kwamba amepona,
alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu;akaanguka kifudifudi miguuni pake,
akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.
b. Jemedari wa kirumi – Mathayo 8:5–13
Kipindi
hiki taifa la Israel lilikuwa chini ya Warumi na tunaona huyu jemedari ambaye
alikuwa mrumi akionekana mwenye Imani zaidi ya yoyote katika israel na mtumishi
wake akaponywa
"Bwana, mimi sistahili uingie chini ya dari
yangu; lakini sema neno tu, na mtumishi wangu atapona."
Hii
inaonyesha kwamba uponyaji hauna kizuizi katika kupokea japo kutunza ni lazima
mtu akubali kuijua kweli na kudumu katika Imani
c. Mwanamke myunani – Marko 7:24-39
Mwanae
anaponywa na pepo kwai le Imani ambayo mama alikuwa nayo
Wayunani
walikuwa watu wa mataifa lakini tunaona wakipokea uponyaji pia kwasababu
aliamini
Kwanini
umzuie mtu kupona kwasababu unamuona wa mataifa ikiwa Yesu aliponya na hao wa
mataifa
Kwanini
ujihesabie hatia wakati Mungu hakuoni hivyo
Nyenyekea
leo na Mungu atakuponya kama alama ya upendo na ukubali kugeuka na kurudi kwake
Mwanamke
myunani
Marko 7:26,29 “Na yule mwanamke ni Myunani, kabila
yake ni Msirofoinike. Akamwomba amtoe pepo katika binti yake. Akamwambia,
Kwa sababu ya neno hilo, enenda zako, pepo amemtoka binti yako.’’
d. Mungu aliponya kuanzia agano la
kale
Katika
agano la kale watu walikuwa hawana neema kama hii ambayo tunayo lakini
kwasababu Furaha ya Mungu ni kuona watu wakipona tunaona akiponya
Yesu
mwenyewe alitumia Mfano wa agano la kale kuhusu NAAMANI,mtu wa mataifa,
akionyesha wazi kuwa Mungu habagui katika uponyaji bali hutazama Imani ya mtu
Luka
4:27 “Tena, palikuwa na wenye ukoma wengi katika Israeli zamani za nabii
Elisha, wala hapana aliyetakaswa ila Naamani, mtu wa Shamu.’’
Ikiwa
uponyaji ulianza tangu agano la kale na tunaona watu wa mataifa wakiponywa pia
basi kizuizi pekee cha kutopokea uponyaji ni KUTOKUAMINI
MIFANO
WA WATU WALIOPONYA AGANO LA KALE
Abimeleki
na Nyumba Yake –
Mwanzo 20:17
Abrahamu
alimuombea Abimeleki, mfalme wa Gerari, na Mungu akamponya yeye, mkewe, na wake
wake wa suria, wakapata kuzaa tena baada ya Mungu kufunga matumbo yao kwa
sababu ya Sara.
Miriam
– Hesabu 12:1–15
Miriam
alipatwa na ukoma baada ya kumpinga Musa. Musa alimwomba Mungu amponye, na
ingawa Miriam alitengwa kwa siku saba, alirudi akiwa amepona.
Hana
– 1 Samweli 1:9–20
Hana,
aliyekuwa tasa, alisali kwa bidii mbele za Mungu, na kupitia maombi yake na
baraka ya kuhani Eli, alipata mtoto, Samweli.
Mfalme
Yeroboamu – 1
Wafalme 13:4–6
Mkono
wa Mfalme Yeroboamu ulikauka aliponyoosha mkono wake kumhukumu nabii. Nabii
huyo alimwombea, na mkono wake ukarejea kuwa mzima.
Mwana
wa Wamama wa Sarepta
– 1 Wafalme 17:17–24
Nabii
Eliya alimfufua mtoto wa mjane wa Sarepta baada ya kufa kwa ugonjwa.
Mwana
wa Mshunemi – 2
Wafalme 4:18–37
Elisha
alimfufua mtoto wa mwanamke Mshunemi aliyekuwa amekufa ghafla.
Naamani,
Jemadari wa SHAmu
– 2 Wafalme 5:1–14
Mtu
Aliyefufuliwa kwa Kugusa Mifupa ya Elisha – 2 Wafalme 13:21
Mtu
aliyekufa alifufuka baada ya mwili wake kugusa mifupa ya nabii Elisha.
Mfalme
Hezekia – 2
Wafalme 20:1–7; Isaya 38:1–8
Hezekia
alipata ugonjwa wa kufa, lakini baada ya maombi yake na ujumbe wa nabii Isaya,
Mungu alimponya na kuongeza maisha yake kwa miaka 15.
Ayubu
– Ayubu 42:10–17
Baada
ya kipindi kirefu cha mateso na ugonjwa, Ayubu aliponywa na kurejeshewa afya na
mali zake baada ya kuombea rafiki zake.
Nebukadneza
– Danieli 4:34, 36
Mfalme
Nebukadneza aliponywa wazimu wake baada ya kuinua macho yake mbinguni na
kumtukuza Mungu wa kweli.
Kumbuka
: ukifatilia uponyaji katika agano la kale utagundua kuwa walioponywa wengi
wala hawakuwa watu wa Taifa la Mungu
Hii
inatokana na kwamba wana wa israel walifika mahali wakawa watu wa kujionyesha
kwamba wanamtumikia Mungu na huo ukawa unafiki mbele za Mungu
Imani
zao zikaharibika kwasababu walijihesabia haki Na kuigiza mbele za watu wa
mataifa na sio kumtumikia Mungu katika roho na kweli
Ushauri
Ikiwa
umepata neema ya wokovu ogopa sana kumzoea MUNGU maana kumzoea Mungu ni kuua
Imani yako
