Kukataa maarifa ni kumkataa Mungu

 


*KUKATAA MAARIFA NI KUMKATAA MUNGU*


✝️✝️✝️✝️✝️✝️✝️✝️


Kuanzia wiki hii unapopiga simu hakikisha pia umeandika semina kama alama ya kumtaka Mungu 


Hii ni kwa faida Yako Ili hata Mungu akikuponya uwe na maarifa ya kutunza ulichopokea


Moja ya sababu ya baadhi ya watu kuutukana ukristo ni kwasababu hawakuambiwa kuhusu UMUHIMU WA maarifa na hivyo Mungu aliwaponya lkn wakarudi wakafungua mlango na kukamatwa tena na mwishoni wakaona Mungu hafanyi wakazoea nguvu za Mungu wakawa watu wa kuombewa kila siku na badae wakaona ni uongo 


Mimi sitaki niwe sababu ya watu kama wewe kukata tamaa na ndio Maana Mungu anataka nitumie muda mwingi kukufundisha


Hakikisha unamtaka Mungu kabla ya nguvu zake Kwa kupenda maarifa (Hosea 4:6) 


Maandiko yanasema Yoyote anayekataa maarifa anamkataa Mungu 


Kitu pekee ambacho uhitaji maarifa ni SALA YA TOBA na baada ya hapo usipofundishwa utaanguka tena maana huna maarifa 


Maarifa hayapatikani Kwa kunywa mafuta au kuombewa bali Kwa neno la Mungu kupitia watumishi wake au Roho Mtakatifu Mwenyew Kwa kusoma neno lake 


*Kila mmoja awe na kiu ya kumtafuta Mungu asije kuona Mungu hafanyi kumbe anajua akifanya utakamatwa tena na hali yako kuwa mbaya zaidi ya kwanza*


2 petro 2:20 


✝️✝️✝️✝️✝️✝️


FRANK BWENGE

MADHABAHUYABIBLIATIMES

Post a Comment

Previous Post Next Post