SEMINA YA NENO LA MUNGU
JINA LA SEMINA: SIRI
YA JINA LAKO
SEHEMU 01: UDANGANYIFU
AU UKWELI KUHUSU MAJINA YA WATU
Transcripted
From : youtube channel @bibliatimes
Jiunge
whatsapp group 0627945434
Haleluya. Karibu sana kwenye
semina mpya. Naitwa Mwalimu Frank Bwenge nakukaribisha.
Hii semina inaitwa siri ya jina lako. Nataka
nikuambie tu ukweli kwamba watu wengi ni wahanga wa majina yao wenyewe. Watu
wengi aina ya maisha wanayoishi, aina ya matatizo wanayokutana nayo, aina ya
vikwazo kwenye maisha yao ni kwa sababu hawaijui siri ya jina lao.
Kwahiyo kwenye hii semina
tutaenda kujifunza siri ya jina lako. Jina ni nini? Na sehemu ya kwanza
nitakufundisha udanganyifu kuhusu majina ambao umeharibu hatima za wengi
Kuna vitu ambavyo vipo mtaani.
Kuna vitu ambavyo vipo ambavyo watu wamevizoea na wanaona ni kawaida. Lakini
nakuambia ni uhadaifu wa shetani kuhusu majina. So lazima ujue hiki kitu
kitakusaidia sana. Sema amen. Kabla hatujaendelea naomba tumshukuru Mungu.
Baba asante kwa ajili ya neema
hii. Asante kwa kibali cha semina hii mpya. Malango ya masaa haya ninaliinua
jina lako na kulitukuza katika jina la Yesu Kristo mnazareti aliye hai. Nenda
pamoja nasi ukatufundishe ukatuelekeze katika jinala Yesu. Ninaomba sasa fahamu
za watu wako eh Bwana zikafunguke kabisa na kila hila za adui zizipate nafasi.
Amen.
Karibu sana sehemu ya kwanza
ambayo inaitwa Udanganyifu Kuhusu Majina Kutoka Kwa Shetani. Unaweza
ukaandika uhadaifu kuhusu majina. Na kuna vitu ambavyo nitakuelekeza leo
ambavyo unapaswa uviandike kama sehemu ya utangulizi yaani sehemu hii ya
kwanza. Na hakika Mungu anaenda kukubadili, anaenda kukuelekeza vitu vingi
sana.
Wengi mpaka hii semina inaisha
tutakuja kugundua kwanza kuna aina ya mamlaka tumeyakosa kwa sababu hatukujua
siri ya majina. Lakini pia tutakuja kugundua kuna aina ya watoto wetu au kuna
aina ya maisha tunaishi kwa sababu kuna siri hatukujua kuhusu majina yetu. Sema
amina. Karibu sana.
Sasa kitu cha kwanza ambacho
unatakiwa ukijue
NAMBA MOJA #01
Ni kwamba kila kitu kina jina.
Kiwe kiumbe hai, kisiwe kiumbe hai kina jina. Kila kitu kina jina. Kila kitu duniani
kina jina
Kama Mungu alikipa kila kitu jina
maana yake Jina ni muhimu sana na jina unapewa sawasawa na ulivyo ,ukikosea
kupewa jina maana haitakuwa kama ulivyo
NAMBA MBILI #02
Jina sio herufi haleluya jina
sio herufi. Kuna watu ambao walichokifanya ni nini? Wakati wanaita majina ya
watoto wao wakachukua jina lao. Jina la baba labda jina la baba anaitwa John
alafu jina la mama anaitwa Dorcas. Alafu yule mtoto akachukua ile “jo”
wakaunganisha na “do” kwa hiyo wakamuita JODO. Haleluya.
Wakamuita nini? Jodo.
Nataka nikuambie kitu kimoja
unaweza kuwa umeunganisha vitu viwili ambavyo huvijui. Yaani nikwambie tu kweli
kama hawa wazazi wana vifungo. John ana kifungo, Dorcas ana kifungo.Ulichofanya
umeunganisha vifungo viwili, matatizo mawili. Lazima ujue kwamba majina sio
herufi tu.
Mtu ambaye anadhani majina ni
herufi atanishangaa. Sasa shida iko wapi?
Very soon nitakuonyesha
kimaandiko kabisa ili uelewe ni nini ambacho tunazungumza hapa ili uelewe. Na
kwenye haya maandiko tutaenda kusimamia mstari kwenye hii sehemu ya kwanza.
Naomba tusimamie mstari ule wa kitabu cha Mwanzo ili ujue kwamba Mungu anaelewa
umuhimu wa majina. Mungu ana utaratibu wa kuwapa majina viumbe hai na visivyo
hai. Na yeyote ambaye hafuati ule utaratibu maanake anajikuta kwenye
changamoto.
Ukisoma mwanzo ya pili kuanzia
mstari wa 19 (Mwanzo 2:10-) inasema Bwana Mungu akafanyiza kutoka
katika ardhi kila mnyama wa msituni na kila ndege wa angani akamletea Adam
ili aone atawaitaje kila kiumbe hai jina alilokiita Adamu likawa ndilo
jina lake.
Kama Mungu alifahamu umuhimu wa
majina nataka nikuambie lazima wewe pia ndani yako ujue kuna umuhimu wa majina.
unaona Mungu anazungumza ili aone atawaitaje maana yake ni nini? Kulikuwa na
namna kama angewaita angeona kuna shida angerekebisha.
So Mungu alisimamia utaratibu mzima wa kuwaita
majina wale viumbe. Sema haleluya.
Lazima ujue Mungu yuko very
serious na majina. na majina sio herufi. Amen. Nitakufundisha mbele hapo kidogo
ili ujue kumbe nyuma ya jina kuna nini. Kitu kingine unapaswa ujue jina
sio swaga.
Jina sio swaga.
Kuna watu walitafuta swaga unaangalia basketball unamsikia tu mchezaji anaitwa TONNYKA
na wewe unaenda unachukua TONNYKA jina tu unaona linasound vizuri unaona
linaswaga kwa hiyo unataka mtoto wako akiwa anaitwa jina lake liwe na utofauti
labda wigos wigos
labda unapenda kusikiliza miziki
ya dunia alafu kuna sauti tu ukiisikanga unapenda labda labda templo
(Haya majina nayatengeneza tu
rafiki yangu sio kwamba yapo. Okay)
Kwa hiyo unasema na wewe mwanangu
nitamuita tempo. Yaani swaga fulani hivi. Kuna mama mmoja alinitafuta alipewa
majina mtoto wake alafu yeye akaona haya mbona hayasoundi vizuri akaongezea
junior
kwa mfano umeenda kwa kwa
mchungaji wako kwa padri amekuombea alafu akakupa jina wewe mwenyewe ulienda
kuomba jina umepewa jina alafu unapewa jina unaanza kuliona halina swaga
tayari kuna shida sehemu hilo
jina litakuja kumtesa huyo mtoto. Sema amina kama unanielewa. So majina
hayatolewi kwa swaga ndugu zangu.
Lakini pia jina sio matamshi
mazuri. Eh kuna mtu anataka matamshi mazuri kwamba mwanangu akiitwa aitike
virahisi. Yaani sio swala la kuitika kirahisi. Sio swala la matamshi magumu. Eh
sio swala hilo. Majina ni zaidi ya hicho kitu.
Nataka nikuambie ukisikiliza hadi
mwisho wa hii semina
utagundua alafu utaanza kuponywa
utafunguliwa kuna vitu utafunguliwa automatic. Haleluya. Lakini lazima ujue pia
kuwa tupo sehemu ya PILI
tumeanza namba moja. Nikakuambia
kila kitu kina jina. Kiwe kiumbe hai, kisiwe kiumbe hai. Kwa sababu kama
havijapewa utambulisho utavijuaje wewe mwanadamu? Utajuaje hili ni jina, hili
ni jini ni ndoo, hii ni kiti? Vyote hivyo vina majina.
Alafu namba mbili nimekuambia
nikakwambia jina sio herufi, jina sio swaga, jina sio matamshi mazuri. Lakini
pia nataka nikuongezee
sehemu hii kwenye namba mbili watu
hawaitwi majina kwa kuiga. hii siri hii unaweza ukasema mtumishi ndio
watu hawaitwi majina kwa kuiga. Sio kwa sababu bibi yako anaitwa hivi na wewe
unachukua jina. Mama YAko anaitwa hivi ni jina hii siri nakuambia kwa sababu
hata mimi sikuijua. umenielewa? Eh.
So Roho mtakatifu anavyoachilia
hili somo Inabidi uwe mtii. Haita make sense hapa mwanzoni lakini nataka
nikuambie nikishaanza kukuonyesha maandiko utakuja uelewe. Maandiko yanafunua
kila kitu na utaelewa vizuri mno. Sawa? Eh.
So lazima ujue watu hawaitwi
majina kwa kuiga. Nikupe ushuhuda wa dada mmoja mama yake akiwa huko ambako
alikuwa kuna jina alilisikia. mamake alikuwa mkristo lile jina wala hakutaka
kufuatilia lile jina ni la wapi of course lile jina lilikuwa ni la kiislamu
ukifuatilia ni moja ya wake wale
wa yule muhammad okay so alivyosikia tu
mama mmoja amemuita mtoto wake pale akasema nikija kuzaa mwanangu nitamuita
hili jina i'm telling alikuja akamuita lile jina lile jina lilimsumbua sana
lilimsumbua
hivi haujawahi kukutana na mtoto
anaitwa kwa jina fulani alafu anaanza kulikataa anaanza kulia.
Do you think huwa ni emergency?
Ni ajali hapana huwa sio ajali huwa sio
ajali so majina hatuiti kwa kuiga. Okay.
NAMBA TATU #03
jina lolote. Jina lolote lina sources
mbili. Yaani jina vyanzo viwili. Yaani jina lolote ambalo utaita. Sawa? Eh lina
vyanzo viwili. Jina lolote ili liwe jina lazima litoke kwenye ufahamu.
Umenielewa? Yaani lazima kuwe na ufahamu fulani. Lazima kuwe na maarifa fulani.
Umenielewa?
Sasa kuna maarifa ya mbinguni
alafu kuna maarifa ya duniani. Jina lolote ambalo limetoka katika maarifa ya
mbinguni yaani ni jina linatoka kwa Mungu. Maanake ni Mungu ambaye anaweza
kutoa jina. Sawa? Eh umenielewa?
jina lolote ambalo haujafunuliwa
na Mungu mwenyewe ni hatari Eh. Sasa Mungu anachofanya nini? Anakupa jina alafu
wewe ndio unampa jina mtoto. Hivi unadhani kwa nini ah malaika alikuja moja kwa
moja na jina la Yesu? Kwa nini malaika walivyoenda kwa Yohana Mbatizaji
walienda na jina la Yohana moja kwa moja?
Kwa sababu Mungu anajua adui anaweza kutumia
chansi ya jina kuharibu kazi nzima. So lazima ujue source au vyanzo vya majina
ni viwili. Aidha kwa shetani au kwa Mungu. Shetani mara nyingi anatumia miungu.
Umenielewa? Eh.
Na hapa lazima uwe makini ili
ujue jina limetoka kwa Mungu. Kama yule mtu ambaye anatoa jina ni mtumishi wa
Mungu kweli ana uhusiano na Roho Mtakatifu. Ukimuomba jina itabidi aidha
atafunuliwa na Roho Mtakatifu pale au achukue kwenye bibilia. Lakini ni vyema
sana ukajua kwamba jina lolote lazima litaweza kuwa na msukumo either wa Mungu
au wa miungu.
Yaani hiyo we don't discuss. Kwa mfano kuna watu
majina yao walipewa na mizimu. Huwezi ukaenda kumuomba jina bibi yako, mama
yako ambaye unajua ana abudu miungu. yeye na waganga yeye na matambiko ni damu
kwa damu. nataka nikuambie lile jina atalipata kwa ufahamu wa kuzimu kwa
ufahamu wa shetani. Kwa sababu mtu yeyote ambaye anamtumikia shetani moja ya
kitu ambacho anakuwa amempa shetani ni nafsi na moja ya kitu ambacho kipo
kwenye nafsi ni ufahamu.
So direct moja ya sehemu ambayo
anakuwa shetani ameishika ni ufahamu. Akiona kuna fursa ya kumkamata mtu
kupitia jina maanake analiachilia moja kwa moja. Mungu pia anaheshimu majina.
Menielewa watoto wa Mungu?
Usije ukadharau jina rafiki yangu. Kuna kuna
baba mmoja na mke wake walikuwa ni walimu wa vyuoni. Ah miaka ya nyuma huko ,wakati
wanaomba wanaomba wakawa wameona jina John. Umenielewa?
unajua baada ya mtoto kujifungua
wakaona John mbona wako wengi sana ,
hapa ndio wazazi wengi wamekamatwa mbona kina
John wako wengi sana kumbuka hili jina limetoka kwa Mungu wenyewe wakaongezea
walimuongezea jina yaani baadala ya kusema John wakamwiita Jordan
Joe waliongezea Yaani kwenye John
wakaongeza swaga ninavyokuambia hizo swaga sasa wakavunja kile Mungu amekisema.
Huyo mtoto baada ya muda aliwasumbua alikuwa anaugua ovyo ovyo ovyo ovyo.
Ukivunja usipomtii Mungu ukamwita jina mtoto ambalo unajisikia wewe umemtii shetani.
jina nimekuambia sio herufi jina
lina siri kubwa. Ndio maana hii semina inaitwa siri ya jina. Mimi
nitakufundisha hapo mbele utaelewa kila kitu.
So namba tatu nimekuambia jina
linaweza likawa na chanzo cha Mungu au chanzo cha shetani. Why? Kutokana na
ufahamu aidha ufahamu wa Mungu au ufahamu uliokamatwa na shetani.
Namba nne #04
Mungu anaheshimu sana majina. Mungu anaheshimu
sana majina. Ukitaka kujua Mungu anaheshimu majina utaona kwenye maandiko
anambadili Abram kuwa Ibrahimu.
Anambadili Simoni kuwa Petro.
Anambadili Sauli kuwa Paulo. Lakini huyu Mungu ukitaka kujua anaheshimu majina
anamuita Adam kwenye Mwanzo 2:19- 20 anamwambia wape majina.
Lakini pia ukitaka kujua Mungu
anaheshimu majina andika ni kwamba yeye mwenyewe ana jina. Haleluya. Yeye ndiye
Mungu. Haleluya.
Na Mungu anaheshimu majina. Kwa
sababu gani? Moja ya kitu ambacho Mungu anakiheshimu ni jina lake. Ukitaka
kujua Mungu hata Mungu anavyokupa huduma
anakupa huduma kwa ajili ya utukufu wa jina lake.
Unajua kipindi cha ufalme wa Hezekia
ufalme wa Ashuru walikuja wakamtukana sana Mungu wa Israeli. Alafu unajua HEzekia
alienda na nyaraka. Unajua alienda kumshtaki na nini? Alishtaki akisema jina
lako wamelitukana.
USICHEZE na jina la Mungu ndio
maana moja ya amri NI usilitaje bure jina LA MUNGU. Maana yake
nini? Jina la Mungu analiheshimu kuliko kawaida. Ulitajitaji tu. Umenielewa?
Sasa sisi tumekuwa wakristo ambao tunaita majina tu ovyo. Unakutana tu na jina
flongo na wewe unamuita mtoto frongo. Unakutana na jina huko shopping na wewe
shopping.
You see
kama Mungu mwenyewe anaheshimu
jina lazima ujue. Sisi alituumba kwenye sura na mfano wake. Kile ambacho Mungu
anapenda lazima tukipende. Asichokipenda hatupasi kukipenda. anachokiheshimu
tunapasa kukiheshimu.
Haleluya.
Ukisoma kutoka 3:14 utagundua
Musa anamuuliza Mungu kutoka 3:14 Mungu akamwambia Musa. Musa baada ya kuuliza
sasa okay ngoja nikusomee hapa juu kuanzia kutoka 3:13- 14 Musa akamwambia
Mungu tazama nitakapofika kwa wana wa Israeli na kuwaambia Mungu wa baba zenu
amenituma kwenu nao wakiniuliza jina lake ni nani niwaambie nini?
Ndio maana kila kitu lazima kiwe
na jina kwa sababu ndio njia pekee ya utambulisho sema haleluya alafu mstari wa
14 Mungu akamwambia Musa mimi niko ambaye niko akasema ndivyo
utakavyowaambia wana wa Israeli, mimi Niko amenituma kwenu.
Haleluya.
Unajua Mungu alikuwa anamaanisha
nini? Hana jina moja. Yeye ni Mungu ambaye anajifunua sawasawa na ulivyomuita.
Yeye ni Mungu ambaye anajifunua sawasawa na wewe ulivyomuita. Ndio maana
ukisoma bibilia utagundua Mungu ana majina mengi na majina yote mazuri
ya utukufu ni majiNa ya Mungu mwenyewe. Sema amina.
So hii sehemu ya kwanza nataka
uelewe hivi vitu vikusaidie na utagundua kwamba Mungu ana majina mengi sana
kwenye Bibilia.
ukianza na anajulikana kama mimi
niko yaani Jehova au Yahwe hilo ndio jina ambalo Mungu anajipa okay
kusoma kutoka 3:14
lakini kuna jina jingine anajiita
Jehova JiRe. Hii utasoma Mwanzo 22:14. Mwanzo 22:14. Naomba nikusomee
haya ni majina ya Mungu. Na muda mwingine angalia shida gani unaipitia. Kwa
mfano unahitaji uponyaji anaitwa Jehova RAPHa maanake Mungu anayeponya.
Ukisoma Mwanzo 22:14 inasema
Ibrahimu akapaita mahali hapo Jehova jiRe kama watu wasemavyo hata leo katika
mlima wa Bwana itapatikana.
Haleluya.
Hii inamaanisha nini? Bwana
atatualizia au Bwana atatupatia mahitaji yetu. Okay. Yes. Kasome.
Ukisoma stori nzuri ya Ibrahimu alivyokuwa anaenda kutoa nini? Kumtoa sadaka
mwanaye. Alafu ghafla Mungu akampatia kondoo. Haleluya.
So alivyokuwa anaenda mtoto wake
alimuuliza baba mbona naona kuni naona kila kitu mwanakondoo yuko wapi? Akasema
Bwana atatuPATia Bwana atatupatia. Haleluya. Haleluya.
So jina la kwanza ni ya ni Yahwe
au Jehova au mimi niko ambao ni kutoka 3:14. Jina la pili ambalo nataka
nikufundishe sitakupa majina yote. Okay. Ah sitakupa majina yote. Ni majina
mengi sana. Okay.
Jina jina jina la pili
nimekuambia ni nini? Ni Jehova JIRE. Jina la tatu ni Jehova Nissi Bwana
ni bendera yangu. Soma kutoka 17:15. Kutoka 1715.
Jina la nne ni Jehova Shalom.
Haleluya. Jehova Shalom. Hiyo ni namba nne. Bwana ni amani yangu.
Hiyo ndio maana yake. Okay? Soma waamuzi 6:24. Na hii ukisoma utaelewa ilikuwa
ni pale ambapo Gideon alipompokea Mungu kama amani yake. Alikuwa mtu ambaye
anajificha. Hata kipindi ambacho malaika anamtokea alikuwa amejificha. So
Gideon baada ya kuona Mungu amemtokea anamtambua kama Bwana ni amani yangu
yaani Jehova Shalom.
Lakini namba tano ni El Shaddai
, Mungu mwenye nguvu zote. Soma kitabu cha Mwanzo 17:1 ndivyo
ambavyo Mungu alijifunua kwa Ibrahimu. Okay.
namba sita. Elohim yaani Mungu
muumba. Ukisoma kitabu cha Mwanzo 1:1 Bibilia inasema hapo mwanzo Mungu
aliziumba mbingu na nchi. Huyu Mungu ukienda kusoma kwenye lugha ya wenzetu
ilitolewa kutoka kwenye neno inaitwa Elohim. Yaani Mungu muumba. Elohim.
Namba saba anajulikana kama Jehova
Adonai. Yaani Adonai Bwana au mkuu. Hiyo ndio maana ya
Adonai. Okay. Na hii inatumika kumaanisha Mungu kama mtawala na Bwana.
Haleluya. Haleluya. Haleluya.
So majina ya Mungu ni mengi. Jina
jingine nikuongezee Jehova TSdikenU. Okay. Maana yake Bwana ni haki yetu.
Hii nikutajie ni T S I D K E N U Haleluya. Haya ni majina ambayo Mungu nataka
nikuonyeshe umuhimu wa majina.
Kama Mungu alijifunua katika
lazima kwanza ujue Mungu ni tofauti. Jina la Mungu ni tofauti na majina mengine
yoyote. Yaani jina la Mungu lenyewe linanyumbulika
kutegemeana na wewe unataka upo
kwenye shida gani ndio maana majina mazuri yote ni ya nani? Ya Mungu. Majina
yenye utukufu yote ni ya nani? Ni ya Mungu.
So najaribu kukupa majina yenye
utukufu
Bwana ni haki yetu. Soma
yeremia 23:6. Yeremia 23:6 mstari wa sita
inasema katika siku zake yake Yuda ataokolewa na Israeli atakaa salama na jina
lake atakaloitwa ni hili Bwana ni haki yetu.
Okay. Sasa kiyahudi maana yake
nini? Kiyahudi ni Jehova Tsdikenu. Okay. Yes. Yaani Bwana ni haki yetu.
Jina jingine ni Jehova Shamah.
Maana yake nini? Bwana yuko hapo. Okay. Ukisoma. Ezekieli 48:35
kuuzunguka ni mianzi 18,000 na jina la mji huo tangu siku hiyo litakuwa hili.
Bwana yuko hapa. Bwana yuko hapa inamaanisha Jehova Shama.
Lakini pia namba 10 I think namba
10 Jehova rohi. Hii ndio ile ile zaburi ya 23 tunaitanga ni zaburi ya
Jehova rohi. Okay. Yote hayo ni majina. So Jehova rohi Bwana ni mchungaji
wangu.
Soma Zaburi ya 23:1. So ukitaka
Mungu ajifunue kama mchungaji wako maanake unamuita kama Jehova rohi. Jehova
rohi. Okay? Lakini kama ukihitaji Mungu ashuke kama mponyaji, yaani Jehova rapha,
Bwana anayeponya utamuita kama Jehova rapha. Okay. Kutoka 15:26. Tusome kutoka
15 26 inasema nini?
Akawaambia kwamba utaisikiliza oh
sorry kutoka 15 kutoka [Muziki] 15 26 yaani yenyewe akawaambia akawaambia
kwamba utaisikiliza kwa bidii sauti ya Bwana Mungu wako na kuyafanya
yaliyoelekea mbele zake yake na kutega masikio usikie maagizo yake na kuzishika
amri zake. Mimi sitatia juu yako maradhi yoyote niliyowatia Wamisri kwa kuwa
mimi ndimi Bwana nikuponyaye. Ndio maana kuna nyimbo inaitanga wewe ni bwana
uniponya maanake ni Jehova Rapha kutoka 15:26 haleluya
kuna Jehova sabaoth bwana
wa majeshi bwana wa vita kasome 1 Samueli 1:3
kuna Jehova Elyon maana yake Mungu aliye juu sana kasome
mwanzo 14:18
El roi mana yake “Mungu
aonaye’ Mwanzo 16:13
Lakini pia Mungu anajifunua kama EL
elom yaani Mungu wa milele. Soma Isaya 40:28.
Alafu kuna mahali anajifunua kama
Jehova qanna yaani Mungu
mwenye wivu. Kasome kutoka 34:14. Haleluya.
Kuna kitu utakuwa umejifunza hapa
kwamba majina pia ni utambulisho majina pia yanazungumzia tabia. Yanasema wewe
ni nani. Ukikosea jina mtoto wako ukamuita taabu. Mh. Ndio taabu
imekuja. Eh.
Nimekuambia cha kwanza namba moja
kila kitu kina jina. Na kama kila kitu kina jina hupaswi kudharau kwa sababu
jina kwa alama ya mwanzoni ni utambulisho tutakujua kwa jina lako. Okay?
Lakini pia nikakuambia kwamba
jina sio herufi, jina sio swaga, jina sio matamshi mazuri. Watu hawaitwi majina
kwa kuiga.
Na namba tatu nikakwambia kutoka
hapo juu kwa sababu hatuiti kwa kuiga. maanake jina lolote either linaweza
kutoka kwa Mungu au kwa shetani. Hamnanga mtu kati. Okay. Nakumbuka haya majina
yote ambaye ataita ni mwanadamu. Maanake Mungu anaweza kutumia mwanadamu.
Shetani anaweza kutumia mwanadamu kuita hayo majina. Haina maana shetani
atakuja kuita majina yeye mwenyewe.
Namba tatu.
Okay. Namba namba tatu ah ni
hiyo.
Namba nne Mungu anaheshimu sana
majina. Nikakuonyesha yeye mwenyewe ana majina. Haleluya. Lakini alimuita Adam
akamwambia wape majina. Lakini tunaona hata Yesu baada ya kufufuka zawadi
aliyopewa ni jina.
Lazima ujue Mungu anaheshimu
majina kiasi gani. Haleluya. Ehe. Eh so Mungu ana majina mengi na wewe ndio
utaamua ajifunue kwa jina lipi? Ndio maana anakwambia Mungu sio mwanadamu.
Umenielewa? Eh yes. Wewe mwanadamu na jina moja lakini Mungu anaweza kujifunua
tofauti.
Haleluya. Haleluya. Hii semina
itakusaidia vitu vingi. Mi nakuambia wewe endelea kunisikiliza hadi mwisho.
Hautabaki hapo ulipo. Okay? Yes.
Hautabaki ulipo hapo.
Mungu wa mbinguni akusaidie sana
sana. Lazima ujue kuyatumia haya majina ya Mungu. Kuna wakati un upo kwenye
vita maanake utamuita kama nani? Sabaoth bwana wa majeshi. Kuna wakati ndugu
yangu umenielewa? Eh. Kuna wakati una magonjwa unapitia shida utamuita kama
Jehova Jehova rapha. Umenielewa?
Kuna wakati utaona kama Mungu
maeneo kama vile Mungu hayupo. Ni kama vile kuna nguvu zingine. Eh hapo unaweza
ukamuita pia kama Jehova Shama. Haleluya.
Hiki kitu kikusaidie wewe kuelewa
unapokuwa unaomba. Ndio maana utakuta wenzio wanatamka maneno mengi kwenye
maombi kwa sababu sometimes ni maarifa kama haya.
Anamuita Mungu kwenye angle
tofauti tofauti tofauti tofauti. Remember unapoita jina huiti herufi.
Nimewaambia sio matamshi unayotamka sio sauti ile inayotoka. Yes.
Nitakufundisha nyuma ya jina kuna roho. Nitakufundisha. Haleluya
. So unapoliita jina la Mungu sifikiri
unaita tu herufi. Hapana. Sema amina.
Yesu anasema maneno niwaambio.
Maneno niwaambiayo ni roho. Maana yake jina ni maneno yanayotoka. Nyuma yake
yana roho. Haleluya. Sio maneno pekee yake. Ni maneno ambayo nyuma yake yana
roho.