SEHEMU YA PILI
MAGONJWA
SIO MAPENZI YA MUNGU
Ukweli ni kuwa bado kuna uongo unatapakaa
kwamba kuna watu wanaumwa kwasababu Mungu amewapa magonjwa
Katika agano la kale Mungu alitumia magonjwa
kama njia ya kuwaadhibu watu yaani kama laana(Kumbukumbu la Torati 28)
kwasababu mauti ilikuwa na nguvu lakini baada ya ufufuo wa Bwana Yesu alivunja
laana zote ikiwepo laana ya magonjwa maana ameshinda mauti
Wagalatia 3:13 “Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa
kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu
aangikwaye juu ya mti;’’
Kusema
kuwa magonjwa ni mapenzi ya Mungu ni kuitukana kazi ya msalaba maana moja ya
sababu ya kwanini Yesu alikuja duniani ilikuwa kuyabeba magonjwa yetu tena kwa
mateso makubwa
Aliyeyabeba
magonjwa ni namna gani anaweza tena kukurudishia magonjwa wewe ?
Bwana
Yesu hawezi kuja duniani kuyabeba magonjwa yetu halafu tena baada ya kufika
mbinguni arudishe kile ambacho alikifia msalabani
1
petro 2:24 “Yeye
mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa
mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa.
Ni
wazi uponyaji ni Sehemu ya mpango wa uponyaji wa MUNGU kwa wanadamu sawasawa na
ilivyo maondoleo ya dhambi
Kusema
magonjwa ni mapenzi ya Mungu nis awa na kusema kwamba Kutenda dhambi ni mapenzi
ya Mungu maana vyote ni Sehemu ya mpango wa ukombozi
Kama
ambavyo unaichukia dhambi ndivyo unapaswa pia kuchukia magonjwa maana vyote
Mungu alivitazama na kutuma mwanae ili tusitende dhambi tena na wala tusiugue
tena
WatU
wengI hawana Imani ya kupona kwasababu ya mafundisho ya uongo kwamba magonjwa
ni mapenzi ya MUNGU
Kuna
ana miaka 10 anaumwa lakini anajipa moyo akidhani kuwa Mungu anamjaribu kumbe
ni kifungo cha adui na kwasababu anadhani ni MUNGU kampa huo ugonjwa hivyo basi
hawezi kuchukua hatua yoyote ya Imani ili kupokea uponyaji
Magonjwa
yaliingia duniani baada ya Adam na Eva kuanguka dhambini
Mungu
hakuwa na mpango wa watu waugue ili wamuogope au kuwajaribu
Siku
ambayo Adam na Eva walikula tunda waliingiza mauti duniani na hii mauti ilikuwa
na magonjwa ndani yake pia na shetani akaanza kuwatesa watu
Ufunuo
1:18 “na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na
milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu.’’
Lakini
baada ya kifo na ufufuko wa Bwana Yesu ile mauti aliishinda na kutupa funguo
sisi wana wa Mungu na hivyo tuna mamlaka ya kuangusha magonjwa na magonjwa
kutokuwa Sehemu ya maisha yetu
1 Wakorintho15:55-57:
“Ku wapi, Ewe mauti, kushinda kwako? U wapi, Ewe mauti, uchungu wako?
“Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati. Lakini
Mungu na ashukuriwe atupaye kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo.’’
Magonjwa
yote yanatoka kwa shetani na MUNGU hawezi kukupa ugonjwa ili kukujaribu
Ikiwa
unasoma nakala hii,Mimi Mtumishi wa Mungu Frank Bwenge nataka ujue kuwa shetani
ni muongo na ukiamini kwamba huo ugonjwa sio mapenzi ya Mungu na kisha ukajua
kuwa IMANI YAKO ITAKUPONYA Basi inuka na uende katika hatima yako
Acha
kulalamika tena kwanini Mungu anakutesa Imnuka ukitambua kuwa uliponywa
msalabani na kinachohitajika ni kukataa kuwa wewe ni mgonjwa maana Mungu
anasema wewe sio mgonjwa bali umepona
Anza
kukiri kwamba kupigwa kwake umepona na wala wewe si mgonjwa (ISAYA 53:5)
SHINDA
UONGO HUU
·
Eti
ukimkosea Mungu anakupa magonjwa x
·
Eti
Mungu akitaka kukuinua kiuchumi anakupa magonjwa x
·
Eti
magonjwa ni njia ya kukajaribu x
Usije
kukubali kwamba ugonjwa wowote umetoka kwa Mungu kwasababu yoyote
Na
kama magonjwa yote yametoka kwa shetani basi hayana uhalali kuwepo katika mwili
wako
Mungu
hawezi kutumia dhambi zako kukupa magonjwa bali shetani hutumia dhambi za watu
kama mlango wa kuwazuia katika mambo mbalimbali ikiwepo na magonjwa
Yesu
na mkoma kuhusu mapenzi ya Mungu
Katika
huduma ambazo Yesu alifanya kuna Sehemu nyingi anaonyesha wazi kwamba sio
mapenzi ya Mungu watu kuugua na wala Mungu hafurahii watu kuugua
Marko 1:40-42: “Akaja kwake mtu mwenye ukoma, akamsihi
akipiga magoti, akamwambia, Ukitaka, waweza kunitakasa. Yesu, akamwonea huruma,
akanyosha mkono wake, akamgusa, akamwambia, Nataka; takasika. Mara ukoma
ukamtoka, akatakasika.”
Ukisoma
hilo andiko juu utagundua kuwa mkoma alianza na swali ili kujua kama ni mapenzi
ya Mungu yeye kuponywa na Yesu anamjibu NDIO ni MAPENZI YA MUNGU
Sasa
kipindi hiki wakoma walionekana wachafu kiroho na kimwili na walionekana kana
kwamba wamefanya dhambi kubwa sana na hivyo walitengwa
Walawi 13:45-46:
"Mwenye ukoma atakuwa na nguo zilizoraruliwa, kichwa chake
kitaachwa wazi, atafunika juu ya mdomo wake na kupaza sauti akisema, Najisi!
Najisi! Atakaa peke yake, nje ya kambi ndipo atakapokaa.
Japokuwa
mkoma huyu alionekana ni mtu asiyefaa lakini tunaona Yesu anamponya
Usijali
pengine kuna muda unajihesabia hatia na kuona kama hutapona kwasababu ya aina
ya maisha ambayo ulikuwa unaishi lakini kama YESU alivyomponya mkoma hata wewe
anaweza kukuponya leo,unapaswa KUAMINI TU
Mungu
anataka tufanikiwe pia katika afya
Huwezi
kuwa Tajiri wa afya ikiwa unateswa na magonjwa na kama Mungu anataka ufanikiwe
katika afya yako maana yake si mapenzi yake kukupa wewe ugonjwa
3 Yohana 2:1 “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo
yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo.
Huruma
kama mapenzi ya MUNGU kuponya
Ukifatilia
huduma ya Yesu utagundua kuwa alianza na kuwahurumia , ni wazi Aliona namna
adui aliwatesa watu hawa na akaugua moyoni mwake
Mathayo 14:14 “Yesu akatoka, akaona mkutano mkuu,
akawahurumia, akawaponya wagonjwa wao.’’
Mungu
hafurahii kukuona wewe unaumwa na wala usidhani ndio unajisadaka kwake kwa
kukubali kuumwa bali unaaibisha kazi ya msalaba na unapaswa kuinuka na
kulidhibitisha neno lake kuwa KUPIBWA KWAKE SISI TULIPONA
Yesu
anakiri kuwa magonjwa ni kazi ya shetani
Matendo
ya mitume 10:38 “habari za Yesu wa Nazareti, jinsi Mungu alivyomtia mafuta kwa
Roho Mtakatifu na nguvu naye akazunguka huko na huko, akitenda kazi njema na
kuponya wote walioonewa na Ibilisi; kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.’’
Tunaona
wazi katika andiko hili kuwa moja ya njia ambayo ibilisi anatumia kuwaonea watu
ni magonjwa
Magonjwa
ni silaha ya shetani na wala sio Mungu
