HAKUNA UGONJWA UNAMPATA MTU BILA KUURUHUSU

 


SEHEMU YA KWANZA

HAKUNA UGONJWA UNAMPATA MTU BILA KUURUHUSU

Ukweli ambao watu wengi hawaujui ni kuwa Mungu alivyomuumba mtu ni wazi na Dhahiri kuwa hakuna chochote kitamuingia bila yeye mwenyewe kusema “NDIO INGIA”

Hakuna ugonjwa wowote ambao unaweza kukupata kama hujauruhusu kwa kusema “NDIO”

Unaweza ukakataa kwamba hujawahi kuruhusu ugonjwa ukuingie lakini lazima ujue ulimwengu wa roho hauongei kwa maneno tu bali kwa HISIA,MATENDOna MAWAZO

Kwasababu shetani anajua hana mamlaka yoyote kwa mwana wa Mungu na hawezi kukudhuru tu kama anavyotaka, basi hutanguliza MTEGO kwanza na kwa kushindwa kuutegua ANAPANDA PANDO lake

Upande wa magonjwa mtego mkubwa bi dalili za mwanzo na hu oni mtego na namna unapokea hiyo taarifa itaamua kunaswa kwako au kushindwa kwa adui

Mithali 6:2 “Basi umetegwa kwa maneno ya kinywa chako, Umekamatwa kwa maneno ya kinywa chako,’’

 

NAMNA TUNARUHUSU MAGONJWA KUINGIA

Kuna njia nyingi ambazo huwa zinatafsiri kwamba tumeruhusu ugonjwa kuingia ndani ya miili yetu

a.      Mawazo

Pale unapohisi dalili yoyote katika mwili wako halafu katika Mawazo ukajiona namna umelazwa au namna unateswa na ule ugonjwa ni tafsiri ya kuruhusu ugonjwa uingie ndani yako

Adui siku zote hutumia dalili na Mawazo yako yakiruhusu dalili hizo basi umeruhusu ugonjwa ,ni vyema kutambua kuwa kama mkristo magonjwa yote aliyachukua Bwana Yesu msalabani na hivyo hayana nafasi kwako

Mathayo 8:17 “ili litimie lile neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema, Mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu, Na kuyachukua magonjwa yetu.’’

Pale unapohisi dalili za ugonjwa Fulani haijalishi umeumwa mara ngapi usikubali Mawazo yako kuona tayari ni mgonjwa maana huko ni kuuruhusu ugonjwa

Yesu anasema kumtamani moyoni mwanamke ni kuzini nae na ndivyo ilivyo unapojiona tayari mgonjwa kabla ya kuugua ni kuugua

Chochote ambacho utakiri na kuamini hicho ndicho kinakuwa

b.      Hisia

Unapokea vipi taarifa ya dalili za ugonjwa Fulani ?

Ukweli ni kuwa namna unapokea taarifa huamua pia kama utaipa nafasi hiyo taarifa au kuikataa isikudhuru

Imagine ,umekaa tu ndani ghafla ukahisi tumbo linauma halafu taarifa hii ukaipokea kwa hofu na kukimbilia kunywa Panadol

Hii inatafsiri tayari umefungua mlango wa tatizo la tumbo kwa njia ya hofu

Ukipokea taarifa mbaya katika mwili wako usiikubali na wala usiogope tumia neno la Mungu kama upanga wa Roho kusambaratisha taarifa hiyo

Isaya 53:5” Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.’’

Ikiwa Yesu alipigwa sana na katika kupigwa nilipona na sio nitapona hii ina maanisha hakuna ugonjwa wenye nguvu juu ya mwili wangu labda kama mimi nitaruhusu huo ugonjwan

Hivi unajua kwanini wagonjwa wa UKIMWI huwa wanakufa baada ya kupima na kujulikana wana UKIMWI?

Hii ni kwasababu ya hofu inapoingia na kuanza kuwaza namna Maisha yao ni mafupi

Hofu na Mawazo ni silaha inayoupa ugonjwa nguvu na kumdhuru mwanadamu

Hofu ni hatari zaidi ya UKIMWI mwenyewe na hakuna ushindi wowote katika hofu

Hofu sikuzote humtoa Mungu na kumfanya kana kwamba hana msaada kwenye maisha ya mtu na hapa ndipo shetani hupata nguvu katika ugonjwa au jambo lolote

Shetani hana nguvu kwa mwanadamu ambayo anatawala Mawazo yake na hana hofu sawasawa na neno la Mungu

Wagonjwa wengi wa UKIMWI walianza kukonda na hata kufa baada ya hofu kuingia kwamba wana UKIMWI japo kabla ya hapo wala hawakuwa na tatizo lolote

Ukweli mbaya ni kuwa jamii imeaminishwa kwamba UKIMWI unaua ,kwahiyo kila anayepokea taarifa ana UKIMWI anawaza kufa lakini Mungu wetu anasema kuwa kwa kupigwa kwake Yesu ,UKIMWI umepona (1 petro 2:24)

Lazima ufike mahali ujue kuwa sisi kama wana wa Mungu hatusikilizi nini dunia inasema bali mbingu inasema nini na ili ujue mbingu inasema nini ,soma neno la Mungu

Tambua jambo hili

Namna unapokea taarifa yoyote inaamua kama utaruhusu tatizo husika au kulikataa

c.       Uovu

Hii ndio sababu pia inayompa nafasi shetani kupanda magonjwa kwa watu wengi

Mungu hawezi kukupa ugonjwa kama adhabu lakini shetani anaweza kutumia uovu wako kupata uhalali wa kukupandikizia magonjwa

Hii ina maanisha kuwa Mungu atakuponya bila kuangalia uovu wako bali Imani yako na ndio maana Yesu aliponya watu kabla hata ya kuokoka

Yesu anadhibitisha kwamba ugonjwa ni mlango wa shetani kupandikiza magonjwa kwa mtu na sio Mungu kumpa ugonjwa mtu

Yohana 5:14 “Baada ya hayo Yesu akamkuta ndani ya hekalu, akamwambia, Angalia, umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi.’’

d.      Maneno unayojitamkia ndani yako

Hii njia adui huwa anaitumia sana kwa watu ambao wameponywa tayari

Na hapa pia huwa anatumia dalili zilezile namna ugonjwa ulianza ,na hii inaweza kuwa maumivu au hali yoyote

Kumbuka zile dalili ni mtego wa wewe ufanye jambo ndipo ugonjwa uingie

Ukweli ni kwamba watu wengi ambao walipona halafu wakaugua tatizo lile lile walifanya makosa yale yale ya kuupa nafasi ugonjwa kwa maneno yao

Kitendo cha kuhisi dalili za ugonjwa wa kwanza na kukubali kwa maneno kama vile “kumbe sikupona’’ au “nimeanza tena kuumwa’’ hii ni ruhusu unatoa ya huo ugonjwa kurudi

Dalili za ugonjwa sio ugonjwa na lazima utamke neno la Bwana na sio kuangalia historia ya kwamba hata mwanzo ulipona ukaugua tena

Watu wengi ambao wanapona na kuugua tena ni kwasababu wameshindwa kushinda maneno ya kujitamkia

Adui anachofanya anakutega kwa dalili Fulani na ukikubali tu anakunasa

Mithali 6:2  “Basi umetegwa kwa maneno ya kinywa chako, Umekamatwa kwa maneno ya kinywa chako,’’

USHUHUDA WA DADA

Kuna dada mmoja niliwahi kumuombea na Bwana akamponya , na kabla sijakutana nae alikuwa anaishi TABORA na kipindi nakutana nae alikuwa amehama tabora

Yeye alikuwa na presha kipindi hicho na ambao walimchezea ni rafiki zake wa kule Tabora na baada ya kuwa amefunguliwa wakawa wanatafuta njia ya kupandikiza tena ule ugonjwa

Walichofanya walimpigia simu halafu wakampa Taarifa ya kifo ya Jirani mwingine ambaye alikuwa anampenda sana japo alikuwa ameshakufa siku nyingi na akaumia kwanini hakupewa taarifa na wakati moyo wake unamuuma ndio muda ambao adui alipanda zile dalili za presha na yeye ndani yake akasema “kumbe sikupona’’ na hapohapo ile presha ikarudi

Hivi unadhani kwanini wachawi au waganga ni lazima wakutishie watakuua kabla hawajakuua?

Hii ni kwasababu wameshindwa kuua kwahiyo wanachofanya wanakupa taarifa ambayo itapanda hofu ili wapate mlango kwa wewe kuanza kuwaza namna unakufa

Shetani sikuzote anatumia taarifa na vitisho kama silaha ya kumfanya mwanadamu aogope au ajiwazie mabaya kama mlango wa kumteketeza

Shetani hawezi kufanya chochote kama wewe mwanadamu hujamruhusu

ZINGATIA HILI

Hakuna jema au baya ambalo litampata mwanadamu kama hajaamini

Marko 9:23 “Yesu akamwambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye.’’

Neno “yote” ina maanisha ya kutoka kwa shetani na ya kutoka kwa Mungu

IMANI yako ni mlango wa kupokea mazuri au mabaya na Imani ni kitu cha kiroho na inaanzia katika kile unakifahamu (Warumi 10:17) - Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo.

Mungu atakuonyesha upo katika jumba kubwa katika ndoto na ili liwezekane hilo atasubiri UAMINI bila kukata tamaa lakini shetani atakuletea dalili za maumivu kwenye tumbo na ukiona kansa na kuamini kansa utapokea KANSA

Huwezi kupokea chochote bila kuamini kiwe kizuri au kibaya

Chagua kimoja kuamini neno la Mungu au kuamini hisia na kile unachokiona au shetani analeta,maana hata ndoto ni lazima iwe sawasawa na neno la Mungu ili kuiamini

 

Umejifunza nini katika Sehemu hii ya kwanza unaweza kutuma ushuhuda wako kupitia whatsapp 0627945434

 


 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Post a Comment

Previous Post Next Post