IBADA ZA MIUNGU
Hizi ni ibada ambazo zinafanywa na wale ambao wamemfanya shetani Mungu wao
Unaweza ukafanya Ibada za miungu au mizimu bila kujua na madhara yakawa yaleyale
IBADA yoyote inafanyika katika madhabahu na kwasababu ni IBADA ni lazima wahusika watoe sadaka
SADAKA katika ibada za miungu ni DAMU ZA WANYAMA kama mbuzi,ng’ombe ,kondoo n,k na kila sadaka inakuwa na maelekezo yake katika ufalme wa giza
Mfano wa Ibada za miungu au mizimu ni MATAMBIKO na MAZINDIKO
Mizimu wanajua sana kujificha kwahiyo ni rahisi kushiriki kwenye ibada za miungu na ukafikiri na sherehe tu ya mwisho wa mwaka
Wachaga ambao wanaenda kila mwisho wa mwaka wengi wao wamejikuta kwenye ibada za mizimu ya koo zao bila hata kujua na ndio maana wazee wapo serious sana na sherehe hizi za mwisho wa mwaka
IBADA ZA MIUNGU ni mlango ambao mizimu hupata nafasi na kuwa na uhalali kupitia maagano ambayo huyafanyika kupitia sadaka ambazo zinatolewa