Isaya 1:19
[19]Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi;
Kanuni ya Mungu iko wazi kwamba hawezi kufanya Chochote kwa mtu ambaye HAJAKUBALI AU HAYUPO TAYARI
Mungu haradhimishi mtu kwasababu alikuumba na UTASHI
KUKUBALI AU KUWA TAYARI haiko ktk maneno bali itaonekana katika matendo
Huwez kusema upo TAYARI MUNGU afanye kwenye maisha yako kama unaishi maisha ambayo HUONYESHI UTAYARI
Huwezi kusema upo tayari Mungu akuponye lkn hutaki kuamka usiku kusali
Huwezi kusema upo tayari Kama hutaki kusikia neno la Mungu
Huwez kusema upo TAYARI kwa Mungu ambaye humtaki
Kumtii Mungu bila kukubali ni unafiki
Yaani kwenda mbele za Mungu akusaidie wakati hujakubali neno lake ni UNAFIKI MBELE ZA MUNGU
Ni sawa na mwanafunz ambaye ameambiwa na mwalimu simama na akasimama lkn ndani yake ANAONA USUMBUFU
Wengi timers ya dhambi za ndani kwa kutokubali japo nje tulionekana kutii
Upo tayari KUPONYWA Lkn neno la Mungu kusikiliza na kujifunza hauko tayari na kuna muda semina za neno la Mungu zinakuudhi na kukuboa
Tengeneza moyo wako ndugu,Mungu hufanya kazi Kwa kanuni na sio mazoea
Utakula mema ya nchi ukiwa tayari lkn pia baada ya kukubali kwanza ndio utii wako itakuwa na matokeo
KUBALI KUJIFUNZA NENO LA MUNGU KAMA ALAMA YA KUMTII MUNGU kisha utapokea uponyaji maana hulituma neno kuwaponya na kuwatoa watu ktk maangamizi
USIKIMBILIE UPONYAJI MKIMBILIE MPONYAJI ambaye ni NENO LA MUNGU
Glory To God 🙏🙏🙏
Mwl Frank Bwenge
MadhabahuYAbibliatimes
✝️✝️✝️✝️✝️✝️✝️✝️✝️